Hamia kwenye habari

JANUARI 15, 2020
PUERTO RIKO

Matetemeko Makubwa ya Ardhi Yatokea Nchini Puerto Riko

Matetemeko Makubwa ya Ardhi Yatokea Nchini Puerto Riko

Januari 7, 2020, tetemeko kubwa lilipiga kisiwa cha Puerto Riko, na matetemeko mengine madogo-madogo yakaendelea. Asubuhi ya Januari 11, kulikuwa na tetemeko kubwa mno.

Kutaniko la Castañer, Lares likiendesha mikutano yao bila umeme

Bado hakuna umeme katika sehemu kubwa iliyoathiriwa, na watu wengi wanaishi nje katika maeneo yaliyo wazi kwa kuwa bado hali si shwari. Halmashauri ya Tawi ya Marekani imethibitisha kwamba hakuna ndugu yetu hata mmoja aliyeumia au kufa. Hata hivyo, ndugu na dada 248 wamebaki bila makao. Kwa kuongezea nyumba 8 zimeharibiwa na nyumba 70 zimepata uharibifu mdogo. Majumba kumi ya Ufalme yameharibika pia. Halmashauri ya Kutoa Msaada iliyoundwa pamoja na waangalizi wa mzunguko wanafanya mipango ya kutoa msaada na kuwafanyia ziara ya uchungaji wahubiri walioathiriwa na janga hilo.

Licha ya changamoto hizi , ndugu zetu wamedumisha ratiba yao ya kiroho. Ndugu Robert Hendriks, anayeratibu jitihada za Dawati la Habari za Umma katika ofisi ya tawi ya Marekani alisema hivi: “Majanga ya namna hii hayatokei mara kwa mara Puerto Riko, hivyo tetemeko hili limewapa mkazo sana ndugu na dada zetu. Hata hivyo, tunatiwa moyo sana kuona bidii yao. Kwa kadiri wanavyoweza wameendelea kufanya mikutano na kuenda utumishi licha ya kukosa umeme na maji. Wazee wanafanya kazi nzuri sana katika ziara zao za uchungaji, kuwatia moyo na kuwasaidia wale wote wenye uhitaji.”

Ndugu wengi wanaishi nje katika maeneo yaliyo wazi ili kuepuka kujeruhiwa na matetemeko mengine

Tunatiwa moyo na jinsi ndugu zetu wanavyonyesha uthamini wa mambo ya kiroho ingawa wanakabiliana na janga lililotokea. Tunasali kwamba Yehova aendelee kuwapa amani ya akili.—Zaburi 119:165