Hamia kwenye habari

UZBEKISTAN

Matukio Muhimu Kihistoria Nchini Uzibekistani

Matukio Muhimu Kihistoria Nchini Uzibekistani
  1. FEBRUARI 19, 2009—Serikali yakataa ombi la 16 la kusajili Mashahidi wa Yehova jijini Tashkent. Maombi ya mapema yalikuwa yamekataliwa pia, yalikuwa ya mwaka wa 1997, 1998, 2000, 2001, 2003, 2004, 2005, na wa 2006

  2. AGOSTI 24, 2006—Serikali yafuta usajili wa shirika la LRO jijini Fergana

  3. AGOSTI 1999—Serikali yasajili upya shirika la LRO jijini Chirchik na shirika la LRO jijini Fergana

  4. MEI 1, 1998—Serikali yatoa sheria ya kudhibiti mashirika ya kidini na inayotaka mashirika hayo yajiandikishe upya

  5. DESEMBA 1996—Serikali yakataa ombi la kwanza la kusajiliwa la Mashahidi wa Yehova jijini Tashkent

  6. DESEMBA 17, 1994—Serikali yasajili mashirika ya kidini ya Mashahidi wa Yehova (LRO) katika jiji la Chirchik na Fergana

  7. DESEMBA 8, 1992—Serikali mpya ilitayarisha katiba mpya inayowahakikishia raia haki za msingi za kibinadamu

  8. SEPTEMBA 1, 1991—Uzbekistan yapata uhuru

  9. Miaka ya 1960—Utendaji wa kwanza wa Mashahidi wa Yehova ulioripotiwa Angren na Chirchik