Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

“Ninawavulia Kofia Nyinyi Nyote”

“Ninawavulia Kofia Nyinyi Nyote”

“Ninawavulia Kofia Nyinyi Nyote”

HIVYO ndivyo Mkatoliki mcha Mungu kutoka Fairhope, Alabama, Marekani, alivyoandika kuhusu vichapo vya Mashahidi wa Yehova na wale ambao wamempelekea.

“Utungaji wa magazeti na habari zilizo katika magazeti Mnara wa Mlinzi na Amkeni! ni bora kabisa,” akasema. “Mimi hufurahi sikuzote wakati baadhi ya watu wenu wanaponiletea nakala za magazeti hayo. Nami huyasoma yote.

“Watu wenu ni wazuri na wana adabu nzuri, nami hufurahi sana kuona watu wakifanya kazi ya Mungu (Yehova) huku wakitabasamu. Wakati uliopita, watoto wadogo wawili walikuja mlangoni pangu na kujijulisha kisha wakanipa magazeti hayo. Niliwashukuru, nikafurahi sana kuona watoto wadogo wakifanya kazi nzuri badala ya kuwa wakorofi.

“Mimi ni Mkatoliki mcha Mungu. . . , lakini ninafurahia kazi kubwa inayofanywa na tengenezo lenu na watu wenu. Nasema kwa moyo mweupe kwamba ninafurahia kikweli magazeti yenu na ninapendezwa sana na watu wenu wanaotabasamu. . . . Ninawavulia kofia nyinyi nyote. Endeleeni na kazi hiyo nzuri.”

Mashahidi wa Yehova pia huandaa vichapo vinavyotimiza mahitaji hususa. Mojawapo ni broshua ya kurasa 32 yenye kichwa Mungu Anataka Tufanye Nini? Katika masomo 16 inatambulisha mafundisho ya msingi ya Biblia na kile ambacho Biblia husema twahitaji kufanya ili kupokea kibali cha Mungu. Ikiwa ungependa kupokea nakala bila malipo, jaza kuponi iliyopo hapa na uitume kwa anwani iliyoonyeshwa au kwa anwani ifaayo iliyoorodheshwa kwenye ukurasa wa 5 wa gazeti hili.

□ Nitumieni nakala ya broshua Mungu Anataka Tufanye Nini? Onyesha lugha unayotaka

□ Tafadhali wasilianeni nami kuhusu funzo la Biblia la nyumbani bila malipo.