Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

“Hutupa Tumaini na Kuimarisha Imani”

“Hutupa Tumaini na Kuimarisha Imani”

“Hutupa Tumaini na Kuimarisha Imani”

PROGRAMU YA KIMATAIFA YA FUNZO LA BIBLIA itolewayo na Mashahidi wa Yehova, hivi karibuni ilihusu funzo la historia ya kale na unabii uliorekodiwa kwenye kitabu cha Biblia cha Danieli ambalo lilifanywa kwa muda wa miezi kadhaa. Hebu ona uthamini ulioonyeshwa katika barua ifuatayo kutoka Poland.

“Kwa muda mrefu, tulitamani kupata uelewevu sahihi wa unabii wa Biblia wa kitabu cha Danieli. Sasa, tamaa hiyo imetoshelezwa. Kichapo cha kusaidia kujifunza Biblia kinachotumiwa, Sikiliza Unabii wa Danieli!, kina hoja sahili, lugha inayoeleweka, na picha zenye kuvutia. Yote hayo huelimisha na kusadikisha. Hilo limeimarisha tumaini letu kwamba kusudi la Mungu litatimizwa kwa wakati wake. Kichapo hiki bora cha kusaidia kujifunza Biblia hutupa tumaini na kuimarisha imani.”

Je, umehangaishwa na mtazamo wa leo wa shaka, ambao umetia ndani uchambuzi usiofaa wa historia ya Biblia? Ikiwa ndivyo, kichapo Sikiliza Unabii wa Danieli! kitakupendeza na kuchangamsha moyo wako. Waweza kuomba nakala ya kitabu hiki kwa kujaza na kutuma kuponi iliyopo hapa kwa anwani iliyoonyeshwa au kwa anwani ifaayo iliyoorodheshwa kwenye ukurasa wa 5 wa gazeti hili.

□ Nitumieni nakala ya kitabu Sikiliza Unabii wa Danieli!

□ Tafadhali wasilianeni nami kuhusu funzo la Biblia la nyumbani bila malipo.

[Picha katika ukurasa 32 zimeandaliwa na]

Ukanda wa nakshi wa Kiajemi: From the book The Coloured Ornament of All Historical Styles; Aleksanda Mkuu: Roma, Musei Capitolini; Silinda: Photograph taken by courtesy of the British Museum