Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Wakili Atafuta Msaada

Wakili Atafuta Msaada

Wakili Atafuta Msaada

Wakili aliyesikitishwa na idadi ya talaka aliandikia ofisi ya tawi ya Mashahidi wa Yehova nchini Brazili hivi: “Wateja wengi wanaokuja ofisini mwangu tayari wameanza kuchukua hatua za kutengana. Inasikitisha sana kuwasikia wakieleza sababu za kutaka kuvunja ndoa zao, huku wakitoa sababu kama vile kukosekana kwa mawasiliano na upendo. Hawafahamu hata kidogo yale mashauri yaliyo katika vichapo vyenu.”

Kwa kuwa aliwajua Mashahidi wa Yehova, wakili huyo aliandika hivi: “Nitafurahi sana mkinitumia vichapo ninavyoweza kuwapa wateja wangu ili viwasaidie kuona uzito wa ndoa, kufikiria tena uamuzi wao, kupatana, na kuwa na maisha yenye furaha.”

Ikiwa ungependa kupata mashauri ya Biblia yenye manufaa yanayoonyesha jinsi ya kufurahia maisha ya ndoa yenye mafanikio, tutafurahi kukutumia kitabu Siri ya Kupata Furaha ya Familia. Kitabu hicho huzungumzia mambo mawili yanayoweza kuwafanya wenzi wa ndoa waishi pamoja kwa furaha na kupata baraka tele. Unaweza kuomba kitabu hicho kwa kujaza sehemu iliyo hapa chini na kuituma ukitumia anwani iliyoonyeshwa au anwani ifaayo kati ya zile zilizoorodheshwa kwenye ukurasa wa 5 wa gazeti hili.

□ Ningependa kupokea kitabu Siri ya Kupata Furaha ya Familia bila malipo. Andika lugha unayotaka.

□ Ningependa kujifunza Biblia nyumbani kwangu bila malipo.