Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Msaada wa Kulinda Watoto Wetu

Msaada wa Kulinda Watoto Wetu

Msaada wa Kulinda Watoto Wetu

Mwaka jana, mwanamke mmoja huko Virginia, Marekani aliandika barua ili kutoa shukrani zake kwa ajili ya kitabu Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu. Alisema hivi: “Kabla wajukuu wangu hawajaenda kulala, wao huniambia hivi: ‘Nyanya, tusomee hadithi fulani kutoka katika kitabu cha Yesu.’ Wajukuu hao wana umri wa miaka 4, 6, na 7, nao wanapenda sana hadithi hizo.”

Nyanya huyo anasema hivi: “Nilisoma sura ya 32 yenye kichwa ‘Jinsi Yesu Alivyolindwa.’ Nilivutiwa sana na sura hiyo kwa sababu baada ya kuzungumzia jinsi Yehova alivyomlinda Yesu, somo hilo linawasaidia vijana wajilinde wenyewe kwa kuwapa shauri linalofaa. Sura hiyo inasema: ‘Mtu yeyote akijaribu kuvichezea, sema kwa ujasiri na kwa sauti kubwa: “Niache! Naenda kukushtaki!”’”

Nchini Mexico, mama mmoja mwenye binti aliye na umri wa miaka mitano anayeitwa Betsaida alisema kwamba amekuwa akisoma kitabu Mwalimu na binti yake kwa mara ya pili. Mama huyo alisema: “Ulimwengu unazidi kupotoka kiadili, nao watoto wetu wanakabili mikazo zaidi. Binti yangu anasema kwamba anashukuru kupata maagizo kuhusu jinsi anavyoweza kujilinda na watu wanaofanya mambo mabaya, kama wale wanaotajwa katika sura ya 32.”

Kitabu hicho chenye kurasa 256 ambacho kina picha maridadi, na chenye ukubwa wa gazeti hili, kimesaidia sana wazazi kufuata mwongozo wa Biblia wa kuwazoeza watoto wao. (Methali 22:6) Masomo yake ambayo yanategemea mafundisho ya Yesu Kristo, yamesimuliwa kwa lugha rahisi, hata hivyo, habari yenyewe inawahusu watu wote. Unaweza kuomba kitabu hicho kwa kujaza sehemu iliyo hapa chini na kuituma ukitumia anwani iliyoonyeshwa au anwani ifaayo kati ya zile zilizoorodheshwa kwenye ukurasa wa 5 wa gazeti hili.

□ Ningependa kupokea kitabu Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu bila malipo.

□ Ningependa kujifunza Biblia nyumbani kwangu bila malipo.