Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Jinsi ya Kufanya Funzo Lako la Biblia Liwe Lenye Kunufaisha na Kufurahisha Zaidi

Jinsi ya Kufanya Funzo Lako la Biblia Liwe Lenye Kunufaisha na Kufurahisha Zaidi

YOSHUA anakabili changamoto fulani yenye kutisha. Lazima aongoze taifa la Israeli kuingia katika Nchi ya Ahadi licha ya hali ngumu na zenye kuogopesha. Hata hivyo, Yehova anamhakikishia kwamba atafanikiwa, na anamtia moyo hivi: ‘Uwe jasiri na imara. Fuata Sheria yangu. Isome mchana na usiku, ili ufuate kwa uangalifu mambo yote yaliyoandikwa humo. Ndipo utafanikiwa na kutenda kwa hekima.’—Yos. 1:7, 8.

Katika “nyakati [hizi] za hatari zilizo ngumu kushughulika nazo,” sisi pia tunakabili hali nyingi ngumu. (2 Tim. 3:1) Kama Yoshua, sisi pia tunaweza kufanikiwa kwa kufuata ushauri ambao Yehova alimpa. Tunahitaji kusoma Biblia kwa ukawaida na kuwa makini kutumia kanuni zake tunapokabili majaribu.

Lakini huenda wengi wetu tukakiri kwamba sisi si wapenzi wa kusoma, na kwamba kujifunza ni jambo gumu. Hata hivyo, kwa kuwa kujifunza Biblia ni jambo muhimu sana, chunguza kisanduku chenye kichwa “ Jaribu Kutumia Mapendekezo Haya” ili uone madokezo yanayoweza kukusaidia kufanya funzo lako la Biblia liwe lenye kunufaisha na kufurahisha zaidi.

Mtunga zaburi aliimba hivi: “Niongoze katika njia ya amri zako, kwa maana ninapendezwa nayo.” (Zab. 119:35) Unaweza kupata furaha nyingi kwa kuchunguza Neno la Mungu. Kuna vito vingi vyenye thamani utakavyopata ikiwa utaendelea kuchimba ili kutafuta hazina za kiroho.

Ingawa hutaongoza taifa kama Yoshua alivyofanya, bila shaka unakabili changamoto fulani za kibinafsi. Hivyo basi, kama Yoshua, jifunze na kushika mambo yaliyoandikwa yaliyokusudiwa kukunufaisha. Utakapofanya hivyo, wewe pia utafanikiwa na kutenda kwa hekima.