Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Je, Mungu Husikiliza Sala Zako?

Je, Mungu Husikiliza Sala Zako?

Unaposali, je, unahisi kweli Mungu anakusikiliza?

BIBLIA INASEMA NINI?

  • Mungu husikiliza. Biblia inatuhakikishia kwamba “Yehova yuko karibu na wote wanaomwitia, wote wanaomwitia yeye katika ukweli. . . . Husikia kilio chao cha kuomba msaada.”​—Zaburi 145:18, 19.

  • Mungu anataka usali kwake. Biblia inatusihi hivi: “Katika kila jambo kwa sala na dua pamoja na kutoa shukrani, mjulisheni Mungu maombi yenu.”​—Wafilipi 4:6.

  • Mungu anakujali wewe binafsi. Mungu anaelewa vizuri kabisa mahangaiko na mikazo uliyo nayo, naye anataka kukusaidia. Biblia inasema: “[Tupeni] mahangaiko yenu yote juu yake, kwa sababu yeye anawajali ninyi.”​—1 Petro 5:7.