Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Majibu ya Maswali ya Biblia

Majibu ya Maswali ya Biblia

Ni nani watakaoenda mbinguni na kwa nini?

Mamilioni ya watu wanatazamia kwenda mbinguni watakapokufa. Yesu alisema kwamba mitume wake waaminifu ndio watakaoishi mbinguni. Kabla ya kufa, aliahidi kuwatayarishia mahali ili waishi na Baba yake aliye mbinguni.Soma Yohana 14:2.

Kwa nini watu walio duniani watafufuliwa na kwenda kuishi mbinguni? Watafanya nini huko? Yesu aliwaambia mitume wake kwamba watakuwa wafalme. Wataitawala dunia.Soma Luka 22:28-30; Ufunuo 5:10.

Je, watu wote wazuri huenda mbinguni?

Katika nchi nyingi, watu wachache tu ndio hutawala. Kwa kuwa Yesu anawafufua watu fulani wakaishi mbinguni ili watawale dunia, tunaweza kutazamia kwamba wachaguliwa hao ni wachache. (Luka 12:32) Biblia inataja idadi ya watu watakaotawala pamoja na Yesu.Soma Ufunuo 14:1.

Yesu amewatayarishia baadhi ya wafuasi wake makao mbinguni. Je, unajua watafanya kazi gani huko?

Mbali na wale wanaoenda mbinguni, watu wengine pia watathawabishwa. Raia waaminifu wa Ufalme wa Yesu watafurahia kuishi milele katika dunia itakayokuwa paradiso. (Yohana 3:16) Wengine wataingia katika Paradiso baada ya kuokoka uharibifu wa mfumo huu mwovu wa mambo na wengine wataingia baada ya kufufuliwa.Soma Zaburi 37:29; Yohana 5:28, 29.