Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Majibu ya Maswali ya Biblia

Majibu ya Maswali ya Biblia

Kristo atarudi akiwa na kusudi gani?

Kabla Yesu Kristo hajapaa mbinguni mwaka wa 33 W.K., aliahidi kwamba angerudi. Alijilinganisha na mtu mashuhuri aliyesafiri kwenda nchi ya mbali kisha akarudi na mamlaka ya kutawala akiwa mfalme. Yesu atarudi ili kuwaletea wanadamu serikali bora.—Soma Luka 19:11, 12.

Yesu atawaletea wanadamu serikali bora

Kristo atarudi akiwa na mwili wa aina gani? Yesu alifufuliwa akiwa kiumbe wa roho asiyeonekana. (1 Petro 3:18) Kisha, akaenda mbinguni na kuketi kwenye mkono wa kuume wa Mungu. (Zaburi 110:1) Baadaye, Yesu aliletwa mbele ya Yehova Mungu, “Mzee wa Siku,” ambaye alimpa mamlaka ya kuwatawala wanadamu. Yesu hatarudi kama mwanadamu, bali kama Mfalme asiyeonekana.—Soma Danieli 7:13, 14.

Yesu atafanya nini atakapowasili?

Yesu atakapofika bila kuonekana pamoja na malaika wake, atawahukumu wanadamu. Atawaangamiza watu waovu na kuwapa uzima wa milele wale wanaomkubali kuwa Mfalme.—Soma Mathayo 25:31-33, 46.

Yesu atakapotawala akiwa Mfalme, ataigeuza dunia iwe paradiso. Atawafufua wafu ili wafurahie kuishi katika Paradiso hiyo itakayokuwa duniani.—Soma Luka 23:42, 43.