Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Tuwasaidie Wale Walio Katika Uhitaji?

Tuwasaidie Wale Walio Katika Uhitaji?

NDUGU François, muzee wa kutaniko katika inchi moja inayoendelea, anaeleza hivi: “Matokeo ya uchaguzi yalipingwa, hilo likatokeza machafuko yenye jeuri, na kulazimisha maelfu ya Mashahidi wa Yehova kukimbia na kuacha nyumba zao. Haikuwa rahisi kupata chakula na dawa, na bei ya vitu hivyo ilipanda sana. Benki zilifungwa, mashine za kusaidia kuchukua feza hazikufanya kazi tena.”

Ndugu wa biro ya tawi walifanya haraka ili kutuma feza na mahitaji ya lazima kwa Mashahidi waliokimbilia katika Majumba ya Ufalme. Vikundi vya wapiganaji vilifunga barabara ili motokari zisipite, lakini kwa kuwa wote walijua kwamba Mashahidi wa Yehova hawajiingize katika siasa, motokari za biro ya tawi ziliruhusiwa kupita.

Ndugu François anaendelea kusema hivi: “Katika barabara inayoongoza kwenye Jumba moja la Ufalme, askari fulani wenye kujificha walipiga motokari masasi. Lakini, masasi ilipita katikati yetu. Tulipoona askari moja, aliyekuwa na silaha katika mikono yake, akija haraka karibu nasi, tuligeuza motokari, na kurudi haraka kwenye biro ya tawi. Tulimushukuru Yehova kwa kuwa sisi wote tulifika salama. Siku iliyofuata, ndugu 130 waliokuwa katika Jumba la Ufalme walifika mahali palipokuwa na usalama. Wengine walikuja kwenye biro ya tawi na tukawatolea mahitaji yao ya kiroho na kimwili mupaka wakati fujo ilimalizika.”

Ndugu François anasema hivi: “Baadaye, biro ya tawi ilipokea barua nyingi kutoka sehemu mbalimbali za inchi hiyo ambazo ndugu na dada waliandika ili kuonyesha shukrani yao ya kutoka moyoni. Kujionea namna ndugu zao kutoka mahali pengine walivyowasaidia, kuliwafanya waendelee kumutegemea Yehova zaidi.”

Wakati wa misiba ya asili ao misiba inayoletwa na wanadamu, hatuwaambie ndugu na dada zetu ‘wajipashe [waote] moto na kula vizuri.’ (Yak. 2:15, 16) Tofauti na hilo, tunajikaza kuwatolea mahitaji yao ya kimwili. Vivyo hivyo, katika siku za mitume, kisha kujulishwa kwamba njaa ingetokea, ‘wanafunzi waliamua, kila mumoja kwa kadiri ambayo yeyote angeweza kutoa, wafanye huduma ya kupeleka misaada kwa akina ndugu waliokuwa wakikaa Yudea.’​—Mdo. 11:28-30.

Sisi watumishi wa Yehova, tuko tayari kusaidia wale walio katika uhitaji wa kimwili. Lakini watu wana lazima ya kuhangaikiwa kiroho. (Mt. 5:3) Ili kuwasaidia watambue uhitaji wao wa kiroho na namna ya kuutosheleza, Yesu aliamuru wafuasi wake wafanye watu kuwa wanafunzi. (Mt. 28:19, 20) Kila Shahidi wa Yehova anatoa wakati, nguvu, na mali yake ili kutegemeza kazi ya kufanya wanafunzi. Tengenezo la Yehova linatumia michango ili kutoa misaada ya kimwili, lakini michango hiyo inatumiwa zaidi sana ili kutegemeza faida za Ufalme na kueneza habari njema duniani pote. Tunapohubiri na kutoa michango, hilo linaonyesha kwamba tunapenda Mungu na majirani zetu.​—Mt. 22:37-39.

Wote wanaotoa michango ili kutegemeza kazi ya Mashahidi wa Yehova ya kuhubiri inayofanywa duniani pote wanapaswa kuwa hakika kwamba michango yao inatumiwa kwa njia nzuri sana. Je, uko tayari kusaidia ndugu zako walio katika uhitaji? Je, una nia ya kutegemeza kazi ya kuhubiri na kufanya wanafunzi? Ikiwa ndiyo, ‘usiwanyime watu mema wanayostahili, mukono wako ukiwa na uwezo wa kuyafanya.’​—Met. 3:27.