Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Tetea Ibada ya Kweli!

Tetea Ibada ya Kweli!

Kwa Ajili ya Vijana

Tetea Ibada ya Kweli!

Maagizo: Fanya zoezi hili katika mazingira matulivu. Unaposoma maandiko, jiwazie ukiwa katika matukio yanayozungumziwa. Wazia kikao. Sikia sauti. Hisi kama wahusika wakuu wanavyohisi. Wazia kwamba masimulizi haya ni halisi kabisa.

Wahusika wakuu: Eliya, Ahabu, na manabii wa Baali wapatao 450

Muhtasari: Eliya athibitisha kuwa Yehova ni mkuu kuliko Baali.

1 CHUNGUZA TUKIO HILI.—SOMA 1 WAFALME 18:17-40.

Ukitumia karatasi tofauti, chora picha inayoonyesha mahali unapofikiria Eliya na manabii wa Baali walikuwa wamesimama, na mahali madhabahu zilipokuwa.

“Unasikia” sauti zipi wakati vurugu inayoelezewa katika mstari wa 26 hadi 29 ilipokuwa ikiendelea?

․․․․․

Unafikiri Eliya anahisi jinsi gani anapozungumza na manabii wa Baali?

․․․․․

2 CHIMBA ZAIDI.

Kwa nini Eliya alihitaji ujasiri wa kuongea na Ahabu na kisha kufanya jambo ambalo liliwaaibisha mamia ya manabii wa Baali? (Dokezo: Soma 1 Wafalme 18:4, 13, 14.)

․․․․․

Ukitumia vifaa vya kufanyia utafiti unavyoweza kupata, fanya uchunguzi kuhusu ibada ya Baali. Kwa mfano, ibada yao ilihusisha mazoea gani? Ibada ya Baali ilikuwa na uvutano gani juu ya Waisraeli?

․․․․․

Unafikiri ni kwa nini Eliya alichimba mtaro kuzunguka madhabahu ya Yehova na kuujaza maji?

․․․․․

3 TUMIA MAMBO ULIYOJIFUNZA. ANDIKA MAMBO ULIYOJIFUNZA KUHUSU . . .

Ujasiri unaohitajika ili kuitetea ibada ya kweli.

․․․․․

Faida ambazo watu wanaoonyesha ujasiri huo wanapata.

․․․․․

NJIA NYINGINE UNAYOWEZA KUTUMIA HABARI HIYO.

Ni katika hali zipi maishani unaweza kuonyesha ujasiri zaidi katika kuitetea ibada ya kweli?

․․․․․

4 NI MAMBO GANI KATIKA SIMULIZI HILI AMBAYO YAMEKUGUSA MOYO SANA, NA KWA NINI?

․․․․․

Ikiwa huna Biblia, waombe Mashahidi wa Yehova wakupe moja, au soma habari zaidi katika intaneti www.watchtower.org

[Sanduku katika ukurasa wa 31]

Habari Kuhusu Kusanyiko la Wilaya

Kuanzia mwaka huu, habari kuhusu tarehe na mahali ambapo makusanyiko ya wilaya ya kila mwaka yatafanywa hazitapatikana tena kwenye gazeti la Mnara wa Mlinzi. Habari hizo zinaweza kupatikana katika Tovuti ya www.dan124.com.