Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

WASOMAJI WETU WANAULIZA . . .

Je, Yesu Alimuahidi Yule Mutenda-mabaya Uzima Mbinguni?

Je, Yesu Alimuahidi Yule Mutenda-mabaya Uzima Mbinguni?

Ulizo hilo linaulizwa kwa sababu Yesu alimuahidi uzima katika Paradiso yule mutenda​-mabaya aliyetundikwa kwenye muti pembeni yake. Yesu alisema hivi: “Kwa kweli mimi nakuambia leo, Utakuwa pamoja nami katika Paradiso.” (Luka 23:43) Ona kwamba Yesu hakusema ikiwa Paradiso itakuwa wapi. Kwa hiyo, je, Yesu alimaanisha kwamba yule mutenda​-mabaya angekutana naye huko mbinguni?

Kwanza, acheni tuchunguze ikiwa mutenda-mabaya huyo alistahili kupata uzima mbinguni. Wanadamu walio na tumaini la kuishi mbinguni wamebatizwa katika maji na kwa roho takatifu na kwa hiyo wanakuwa wanafunzi wa Yesu waliozaliwa kwa roho. (Yohana 3:3, 5) Jambo lingine ambalo wanaombwa ni kuishi kulingana na kanuni za Mungu za mwenendo muzuri na kuonyesha sifa kama vile uaminifu, utimilifu, na huruma. (1 Wakorintho 6:9-11) Tena, wanapaswa kubaki waaminifu kwa Mungu na Kristo mupaka mwisho wa maisha yao duniani. (Luka 22:28-30; 2 Timotheo 2:12) Ni kwa kutimiza tu mambo hayo yanayoombwa ndipo wanaweza kustahili kufufuliwa na kupewa madaraka mazito yanayowangojea huko mbinguni, ni kusema, kutawala juu ya wanadamu kwa miaka elfu moja wakiwa makuhani na wafalme pamoja na Kristo.​—Ufunuo 20:6.

Tofauti na hilo, yule mutu aliyetundikwa kwenye muti pembeni ya Yesu alikuwa mutenda-mabaya maisha yake yote na alikufa akiwa mutenda-mabaya. (Luka 23:32, 39-41) Kwa kweli, alionyesha mutazamo wa heshima alipomuambia Yesu hivi: “Unikumbuke utakapoingia katika ufalme wako.” (Luka 23:42) Lakini, mutenda-mabaya huyo hakuwa amebatizwa na kuwa mwanafunzi wa Yesu aliyezaliwa kwa roho, wala hakuwa amejionyesha kuwa mutu mwema na mwaminifu maisha yake yote. Je, ni jambo la akili kusema kwamba Yesu alimuahidi kutawala huko mbinguni pamoja na wafuasi wake waaminifu ambao walionyesha ushikamanifu wao kwake?​—Waroma 2: 6, 7.

Kwa mufano: Ikiwa mwanaume fulani anakuomba umusamehe kwa sababu aliiba feza zako, unaweza kuamua kutomushitaki. Lakini, je, unaweza kumutumainia ili aongoze biashara yako ao kumuacha ashugulikie familia yako? Ni watu ambao unatumainia sana ndio unaweza kupatia madaraka kama hayo, sivyo? Vivyo hivyo, wale wanaopewa tumaini la kuishi mbinguni wanapaswa kujionyesha kuwa wanatumainika, na kwamba watatetea kanuni za Mungu za haki wakati watawatawala wanadamu. (Ufunuo 2:10) Ijapokuwa yule mutenda-mabaya alijionyesha kuwa mwema katika dakika za mwisho za maisha yake alipomusihi Yesu, hakuwa ameonyesha kabisa katika maisha yake kwamba alikuwa mutu mwenye kutumainika.

Lakini, je, Yesu alimuambia yule mutenda​-mabaya kwamba atakuwa naye huko mbinguni siku hiyohiyo? Haingekuwa hivyo, kwa sababu Yesu mwenyewe hakuenda mbinguni siku hiyo. Lakini, alikuwa “katika moyo wa dunia,” ni kusema, katika kaburi kwa muda wa siku tatu. (Mathayo 12:40; Marko 10:34) Hata kisha ufufuo wake, Yesu alibaki duniani kwa muda wa siku 40 mbele ya kupanda mbinguni. (Matendo 1:3, 9) Kwa hiyo, yule mutenda-mabaya hangekuwa mbinguni pamoja na Yesu siku hiyo.

Basi, mutenda-mabaya huyo aliahidiwa kuingia katika Paradiso gani? Atakapofufuliwa, ataingia katika Paradiso duniani, ambayo Yesu atatawala. (Matendo 24:15; Ufunuo 21:3, 4) Ili kujua mengi juu ya Paradiso hiyo na mambo ambayo Mungu anatuomba tufanye ili kuingia humo, zungumuza na Mashahidi wa Yehova.