Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Sean Gladwell/Moment via Getty Images

MUENDELEE KUKESHA!

Makuta Yenye Inatumiwa mu Dunia Yote kwa Ajili ya Jeshi Inapita Dola Trilioni Mbili​—Biblia Inasema Nini?

Makuta Yenye Inatumiwa mu Dunia Yote kwa Ajili ya Jeshi Inapita Dola Trilioni Mbili​—Biblia Inasema Nini?

 Mu mwaka wa 2022, serikali za mu dunia zilitumia dola za Amerika trilioni 2.24 kwa ajili ya jeshi; ni mara ya kwanza makuta ya mingi vile inatumiwa kwa ajili ya jeshi. Sababu kubwa ya ile garama yote ni juu Urusi ilishambulia Ukraine. Kulingana na ripoti ya Mwezi wa 4, 2023 ya Institut international de recherche sur la paix de Stockholm (SIPRI), mu mwaka wa 2022:

  •   Makuta yenye ilitumiwa mu Ulaya kwa ajili ya jeshi “iliongezeka kwa asilimia kumi na tatu (13%) mu ile mwaka, ni mara ya kwanza mu Ulaya garama iongezeke vile mu mwaka, tangu mwisho wa vita ya baridi mu 1991.”

  •   “Inakadiriwa kama Urusi…iliongeza garama yake kwa asilimia 9.2, ile inafanya ikiwe inchi ya tatu yenye kutumia makuta mingi sana mu dunia, haiko tena inchi ya tano.”

  •   Amerika njo ingali inchi ya kwanza kutumia makuta mingi sana kwa ajili ya jeshi, “39% ya makuta yenye inatumiwa mu Dunia yote kwa ajili ya jeshi inatolewa na Amerika.”

 Dr. Nan Tian, mwenye alisaidia kuandika ripoti ya SIPRI alisema hivi: “Kuongezeka kwa garama kwa ajili ya jeshi mu dunia yote katika miaka ya hivi karibuni kunaonyesha kama tunaishi mu dunia yenye haina usalama.”‏

 Biblia ilitabiri kama leo serikali kubwa-kubwa za mu dunia hazitaelewana, na inaonyesha tumaini tu moya ya kupata amani.

Biblia ilitabiri kama mapigano kati ya majeshi itaongezeka

  •   Biblia inaita wakati wenye tunaishi leo kuwa “wakati wa mwisho.”​—Danieli 8:19.

  •   Kitabu ya Danieli ilitabiri kama mu ile wakati serikali kubwa-kubwa za dunia zitashindana. Zile serikali ‘zitasukumana,’ ao kupigania utawala. Ile mapigano itatia ndani kutumia “hazina” nyingi sana, ao feza mingi.​—Danieli 11:40, 42, 43.

 Ili kujifunza mambo mingi juu ya huu unabii wa Biblia wa kushangaza, angalia video Unabii Wenye Umetimia​—Danieli Sura ya 11.

Namna tutapata amani ya kweli

  •   Biblia inasema kama Mungu atatosha serikali za wanadamu. “Atasimamisha ufalme wenye hautaharibiwa hata siku moja. Na ufalme huo hautapewa watu wengine wowote. Utaponda na kumaliza falme hizi zote, na ufalme huo peke yake utasimama milele.”​—Danieli 2:44.

  •   Hivi karibuni Yehova a Mungu atafanya jambo yenye wanadamu hawawezi kufanya, ni kusema, ataleta amani ya kweli na yenye haitakuwa na mwisho. Atafanya vile namna gani? Ufalme wake wa mbinguni utaharibu silaha zote na utamaliza jeuri yote.​—Zaburi 46:8, 9.

 Ili kujifunza mengi zaidi juu ya mambo yenye Ufalme wa Mungu utafanya, soma habari “Chini ya Ufalme wa Mungu ‘Amani Itakuwa Nyingi.’

a Yehova ni jina ya pekee ya Mungu.​—Zaburi 83:18.